Ingia
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
🚀 Jiunge na Changamoto yetu ya Ramadhani!
Jifunze zaidi
Ingia
Ingia
Taarifa ya Sura
064

Sura At-Taghaabun

Aya:

18

Mahali iliteremshwa:

Madina

SURAT ATTAGHAABUN 

(Imeteremka Madina)

Imeanzia Sura hii kwa kueleza kuwa kila kiliomo katika mbingu na katika ardhi kinamtakasa Mwenyezi Mungu na kisio laiki na utukufu wake, na kwamba Yeye ndiye Mwenye Ufalme na Mwenye sifa njema zote, na kwamba Yeye ni Muweza wa kila kitu. Kisha hayo yakafuatilizwa kutajwa baadhi ya dalili za utimilivu wa uweza wake na ujuzi wake. Kisha Sura ikatupa macho kuwaangalia makafiri walio kabla ya hawa, na wakawaasi Mitume na Mola Mlezi, na kwamba wao walionja matokeo maovu ya vitendo vyao. Na hayo yalikuwa hivyo kwa sababu Mitume wao walipo kuwa wakiwajia kwa hoja, waliwakataa na wakawapuuza! 

Sura tena ikaingia baada ya hayo kuvunja madai ya makafiri kwamba wao ati hawatafufuliwa. Na ikawataka watu wamuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na Nuru iliyo teremshwa juu yake. Na ikawahadharisha na Siku ya Mkusanyo, siku kutapo dhihiri kupunjana kwa watu. Kwani wale walio amini na wakatenda mema watapata kufuzu kukubwa, na walio kufuru ndio watakuwa watu wa Motoni, na hayo ndiyo marudio maovu. Na hakika masaibu yatakuwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, na hakiki mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu ndio anauongoa moyo wake.

Sura inawataka watu wamtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Wakipuuza, basi hakika Mtume hana juu yake ila kufikisha Ujumbe. Na inawaambia Waumini kuwa mali yao na watoto wao ni fitna, majaribio. Basi isiwe kuyashughulikia hayo kukawapelekea kuacha waliyo amrishwa. Kisha ikawaamrisha wamche Mwenyezi Mungu kwa kadri wawezavyo. Na Sura ikakhitimisha kwa kuwakhusisha Waumini watoe katika nia za kheri, na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kushukuru, Mpole, Mjuzi wa yaliyo fichikana na yanayo onekana. Basi atawalipa kwa mali yao wanayo yatumia. Na kwamba Yeye ni Mwenye nguvu asiye shindilka, Mwenye hikima hafanyi upuuzi.

He has revealed to you ËąO ProphetËş the Book in truth, confirming what came before it, as He revealed the Torah and the Gospel
— Dr. Mustafa Khattab, the Clear Quran
Notes placeholders
Soma, Sikiliza, Tafuta, na Tafakari Qur'ani

Quran.com ni jukwaa linaloaminika na linalotumiwa na mamilioni duniani kote kusoma, kutafuta, kusikiliza na kutafakari kuhusu Qur'ani katika lugha tofauti. Inatoa huduma za tarjuma, tafsiri, vikariri, tarjuma ya neno kwa neno, na zana za ufahamu wa kina, kuifanya Qur'ani ipatikane na kila mtu.

Kama mbinu ya Sadaqah Jariyah, Quran.com imejitolea kusaidia watu kuunganishwa kwa kina na Qur'ani. Ikiungwa mkono na Quran.Foundation , shirika lisilo la faida la 501(c)(3), Quran.com inaendelea kukua kama rasilimali ya bila malipo na yenye thamani kwa wote, Alhamdulillah.

Chunguza
Nyumbani
Redio ya Qur'ani
Wasomaji
Kutuhusu
Watengenezaji
Sasisho za Bidhaa
Maoni
Msaada
Miradi Yetu
Quran.com
Quran For Android
Quran iOS
QuranReflect.com
Sunnah.com
Nuqayah.com
Legacy.Quran.com
Corpus.Quran.com
Miradi isiyo ya faida inayomilikiwa, kusimamiwa, au kufadhiliwa na Quran.Foundation
Viungo Maarufu

Ayatul Kursi

Yaseen

Al Mulk

Ar-Rahman

Al Waqi'ah

Al Kahf

Al Muzzammil

Ramani ya tovutiFaraghaSheria na Masharti
© 2026 Quran.com. Haki Zote Zimehifadhiwa